Wednesday, December 07, 2005

SIRI

Shhhhhh!.....tulia… Sikia nikupe siri ya siri. Naomba fanya hisani uitunze hii siri. Usiende ukisema kila mtu aifahamu siri. Na neno likienea mitaani nitajua nani aliosema na sitosita kukumaliza. Kwa siri.
1
Mipango ya kifo chako nitaifanya kwa siri. Watekelezaji wa kifo chako sitawaomba hisani kuificha siri kama nilivyokuomba wewe. Hao wataapa kiapo. Cha siri.
1
Wananijua. Na wanazijua nguvu zangu, na sheria nilizoweka kuificha siri. Hii siri yetu ya watu wawili. Kumradhi… siri ya watu mia.
1
Ndio najua. Lakini nimeamua hili jambo kulifanya siri. Kwamba siri zangu zinafananafanana na zenu kwa upande mmoja, vile zina asili ya aibu, ukatili, uongo, ujinga, makosa na dhalimu nyingine nyingine.
1
Lakini! lakini, lakini… mie siri zangu zina tofauti kubwa moja na zenu – siri zangu japo zinafanana na zenu mie nafanya yote haya ili kuleta mazuri. Sina nia mbaya asilani. Yote ninayofanya nayafanya ili kuleta mazuri kwetu sote. Na ndio maana nnataka muifiche hii siri.
1
Kwamba uhuru wa vyombo vya habari ni neno tu la kuwalaghai nyinyi mlioko mbali na jukwaa letu watawala. Huku kwetu uhuru wa vyombo vya habari hauruhusiwi kuvuka mipaka kutuingilia nguoni. Mimi pamoja na bunge letu la Uingereza tunayo sheria – Official Secrets Act - Na atakayevunja sheria hii , kama wale waliotoboa siri yetu mimi na bwana Bush ya kutaka kulipua kituo cha habari cha Al Jazeera, tutamkabili kisirisiri mpaka aache kazi ya kutangaza habari.
1
1
Na pale tulipoanzisha vita na mauaji ya hila kama huko Iraki, tutanunua vyombo vya habari kwa siri ili waongope na waendelee kutupigia propaganda ili kutufichia siri yetu.
1
Na wanahabari wakiendelea kutuelemea na utoboaji siri tutaanza kupayuka na kuwapakazia, mshirika wetu Rumsfeld ng’ambo ya Marekani keshaanza. Namtakia kila la heri.
1
Lakini kamwe hatutaungana mkono na serikali ya Tanzania kufungia gazeti la daima – kisa kumkejeli rais? Hatutaungana mkono na Serikali ya Tanzania kwa sababu serikali hiyo haifanyi dhalimu (kama tunavyofanya sisi huko nchi za umangani) ili kuendeleza demokrasia na kurekebisha hali za wananchi. Serikali ya Tanzania haiwatakii watu mema kama tunavyofanya sisi.
Fanya hisani. Tafadhali usiende mitaani kuwaeleza wengine hii siri – hakuna uhuru wa kweli wa vyombo vya habari.