Tuesday, November 06, 2007

RISING VOICES

Kama unapenda kusaidia wengine wajue jinsi ya kublogu ili kuhabarisha umma au kuweka video kwenye mtandao Rising voices wanaendelea kutoa kutoa senti zitakazokurahisishia kufundisha wengine.

Unaweza ukapata dola 5000 zitakazokuwezesha kufundisha wengine. Unachotakiwa kufanya ni kutuma maombi kwa jamaa wa raising voices. Mstari mfu ni novemba 30, 2007.

Fanya utume. Bofya hapa kwa maelezo zaidi. Fomu za maombi zipo mwishoni mwishoni mwa ukurasa.

Mtazamo mbadala: Shivji ahoji tuzo ya Mo Ibrahim

Kwenye kurasa za Pambazuka kuna mawazo mbadala ya Profesa Shivji kuhusu tuzo ya utawala bora aliyopewa Chissano. Na kabla ya Shivji kupandisha makala yake, mwanazuoni Horace Campbell alikwishapandisha nyingine siku chache kabla.

pamoja na mengi mengine Shivji anaanza:

"Mo Ibrahim’s prize for a retired African president which was awarded to Joachim Chissano of Mozambique was in my view an insult to the African people." Issa Shivji raises a number of questions around the award such as how and what is "good governance" and why is it only applied to Africa? And most importantly "for which and whose democracy they are getting a prize".



Horace Campbell kaandika kirefu zaidi:

According to the media, "Mo Ibrahim, a Sudanese-born telecommunications entrepreneur, established the prize as a way of encouraging good governance in a continent blighted by corruption and a frequently loose adherence to democratic principles." Not a word is mentioned about the living conditions of the people of the Sudan from where Mr. Ibrahim hails…..

But, isn’t this prize also a sign of the political retrogression in Africa? The idea of a President voluntarily stepping down is now so novel in the face of leaders such as Museveni and Mugabe that Chissano indeed stands out. Compared to Robert Mugabe and Thabo Mbeki, and their megalomanic policies, Chissano does look good.

While announcing Chissano as the winner, Kofi Annan may have gone overboard by saying, "leadership should be the ability to formulate a vision and to convince others of that vision. It should be the skill of giving courage to accept difficult changes to make possible a longer term aspiration for a better and fairer future."

Sunday, September 23, 2007

TOA MAONI - PENDEKEZA BLOGU BORA AFRIKA


Wanablogu - Msisahau kutembelea katika blogu ya JUMUWATA ilikuchangia, kukosoa, kuongezea na kuupa muelelekeo mkamilifu muelekeo wa JUMUWATA.


Dondoo za katiba ziko ndani ya blogu ya JUMUWATA, hivyo maoni ya wengi yanahitajika ili isije ikawa ni watu wachache wameamua tunaenda wapi.


Mchango wa wanablogu wenye blogu na wasio na blogu unahitajika ilikuwa na kitu kikamilifu kabla ya kwenda kwenye hatua nyingine.




Mapendekezo ya blogu bora Afrika yanafikia mstari mfu tarehe 30 mwezi wa Tisa.


Katika mapendekezo kutoka kila pande za dunia Afrika haina blogu zilizopendekezwa - wakati nikiandika. Kuna ukame kwenye nchi za Afrika - hakuna hata alama moja ya blogu iliyopendekezwa.


Kama kuna blogu inayoandikwa na Mwafrika ambayo inakukuna moyo fanya uipendekeze ndani ya ukurasa huu.


Hapa chini ni maelezo ya kimombo:


Best of the Blogs: Deutsche Welle
Nominate your favorite blogs today! You're a blogger? You know a good blog? You like blogs, videoblogs and podcasts and want to share your favorites with the world?


Well, you've come to the right place. The BOBs -- short for the Best of the Blogs -- are here to keep track of the world's most interesting Weblogs, podcasts and videoblogs, and we need your help in doing it.


Suggest your favorites


You have until September 30 to head over to the suggestion form and give us the lowdown on all the blogs that glue your eyes to the screen and the podcasts that make you keep your headphones on. You can choose from the following categories:


Best Weblog, Best Videoblog, Best Podcast, the Blogwurst Award, Best Weblog /(Insert contest language here) and the Reporters Without Borders Award. In addition to the overall world's Best Weblog, another award will be given to the Best Weblog in each of the BOBs' 10 official languages making for 15 different prizes.


Who gets to play along?


The Deutsche Welle's Best of the Blogs awards are open to any blog, podcast or videoblog in Arabic, Chinese, Dutch, English, French, German, Persian, Portuguese, Russian or Spanish and meet the criteria. Read through the Road Map to find out more of the competition's details.


The people making the decisions


First and foremost, the BOBs are about the Weblogs (and 'casts) you submit, a blog you that is never entered into the contest can never win -- so get to work. When the submission window closes on Sept. 30, the BOBs jury of bloggers, podcasters, journalists and media experts will begin their work.


If your not impressed with the jury members' biographies, then keep an eye on the BOBs Blog, where they will have a chance to stun you with their insight and analysis. And please also check out the sponsors and media partners who are helping make the third annual Best of the Blogs possible.

Thursday, September 13, 2007

Madhumuni ya tangazo la biashara kwanza ni kuvutia na kushika jicho la mnunuzi. Kwa hilo jamaa wa American Apparel wameweza - kushika jicho.

Cha kushangaza, hivi hawakuweza kupata mrembo mkubwa kwa umri kidogo, halafu akasitiri kidogo kifua chake, ambaye wasingempaka masizi kumfanya awe mweusi tii. Nijuavyo Marekani kuna weusi tii kwa wingi.

Sina hakika mlengwa wa biashara hii ni nani, japo tangazo limezua gumzo.

Tuesday, August 28, 2007

MWANZO WA MWISHO WA SIASA ZA RAFU?

"Zitto amekuwa Zitto, wapinzani sasa wamepata hoja, wametuzidi katika hoja, tunapaswa kuchagua viongozi walio bora ili (wapinzani) wasituzidi katika hoja.

"Inashangaza Zitto ambaye amepewa ‘red card’ bungeni kushabikiwa na idadi kubwa ya Watanzania wakiwemo wana CCM ambao walikwenda Jangwani kumlaki na kumsikiliza wakati akitokea Dodoma, ni lazima tukisafishe chama ili wapinzani wasije kutupiku,"

- Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Kapteni Jaka Mwambi
DAIMA, 27-08-2007
Hoja bin hoja kama hivi tutafika kwenye hoja bin haki, akina Zitto wasikome kuzua hoja tutoke kwenye siasa za pilau anazosema JK hapa.

Sunday, August 19, 2007

Australia imefukuza watoto wa viongozi wa serikali ya Zimbabwe

Hatimaye serikali ya Australia imeitikia wito uliotolewa mwezi wa nne mwaka huu na gazeti la Zimdaily, wa kuwafukuza watoto wa viongozi wa serikali ya Zimbabwe ambao wanasoma ughaibuni kama njia mojawapo ya kuwaadhibu viongozi hao.

Adhabu hiyo imetolewa wakati viongozi wa SADC huko Zamnbia wakiwa wakikubaliana kwamba hali ya Zimbabwe sio mbaya kama wamagharibi wanavyodai. Maamuzi ya Australia na yale ya viongozi wa SADC yanafuatana kama vile mabodia wanavyotupiana masumbwi moja baada ya jengine.

Wakati zoezi la kuwataja kwa majina, pamoja na anwani za wanapoishi watoto wa viongozi wa serikali ya Zimbabwe lilipozuka mwezi wa nne mwaka huu - zoezi liliondaliwa na gazeti la Zimdaily msimamo wangu ulikuwa: sioni haki ya binaadamu mmoja kushinikizwa kwa kutumia binadamu mwingine. Kwamba ikiwa baba yangu ana makosa fulani basi na mimi nihukumiwe kwa makosa yale.

Nilitundika maoni pale kwa Jikomboe, wengine walikuwa na mawazo tofauti. Nikichukulia mfano, kama mimi ningekuwa mmojawapo wa watoto wale, mwenye mawazo tofauti na baba yangu, pengine nimetumia skolashipu iliyoangalia uwezo wangu wa kimasomo, na ninafanya vizuri tu shuleni, halafu nizuiwe kuendelea na masomo kwa sababu baba yangu anafanya kazi serikalini… Haki yangu ya kuishi kama mtu huru itakuwa iko wapi.

Ninaelewa haki ya taifa lolote kuwa na uamuzi ni nani anayeweza kuishi katika mipaka yake nabaki na tatizo la kuelewa dhana ya haki za kibinadamu katika hili.

Friday, July 20, 2007

FIMBO YA MBALI INAUA NYOKA

Fimbo ya mbali inaua nyoka. Hizi zama za teknolojia za mitandao ya intaneti zinabadili mambo.
1
Jioni hii baada ya kazi nafungua barua pepe nakutana na tangazo la mkanda mfupi wa muziki wa Ras Nas. Na hivi ndiyo kwanza nimemaliza kuangalia na kusikiliza muziki wa Ras Nas - muwakilishi wa sanaa toka Tanzania.
1
Muziki timilifu kila upande. Anaanza kwa muziki mwororo wa miondoko laini ya rumba ila sebene lililofuata limeniamsha kitini. Ningekuwa na utaalamu wa youtube kama Kitururu ningepandisha filamu. Lakini si haba, kuna kiungo hapa ukibofya utafika kwenye hiyo filamu ya Ras Nas.
1

Halafu nasoma barua pepe nyingine nakutana na kiungo kingine cha muziki wa Tanzania: Chemundu & Mbega Arts. Japo hakuna filamu ya kikundi wala sauti kwenye tovuti - napata ujumbe kuwa sanaa Tanzania inatokota kisawasawa. Kwa maelezo yao:
1
Chemundu na Mbega Arts ni kikundi cha muziki wenye vionjo vya muziki jadi(asili) halisi wa Tanzania na pia kuchanganya na mitindo ya Kimataifa kama:pop,afro rhumba na afro jazz.
Mbega Arts ilianziswa na mwanamuziki maarufu Che Mundugwao " chem ". na kujumuisha wanamuziki na wasanii wa muziki wa jadi vijana wenye vipaji vya hali ya juu ,ambao wameshawahi kushiriki katika ziara na matamasha mbalimbali ya kitaifa(tamasha la sanaa Bagamoyo) na kimataifa katika nchi za Kenya,Sweden,Denmark,Finland,Uingereza.n.k
1
Hiyo isitoshe, ndani ya barua pepe nyingine nakuta jamaa wa Afropop Worldwide wanaitangaza Tanzania kinamna. Moja ya santuri wanazocheza katika juma la muziki wa Afrika (African Summer Dance Party) inatoka kwa bendi ya Tanzania FM Academia. FM wamewekwa bega kwa bega na Hugh Masekela na Ricardo Lemvo katika chaguo la wataalamu wa AfroPop.
1
Nimeshapata mshawasha, ngoja nielekee kwenye miziki mjini - kuna rege mitaa ya kati huko. Ijumaa hii silali ndani. Fimbo ya mbali ishanichapa.

Tuesday, June 26, 2007

Nyerere Press Conference - 14 March 1995

"Any government that works for the wealthy does not collect tax, it chooses to harass small-time dealers,"

"Corruption in Tanzania has no bounds. Every country I visit they talk about corruption in Tanzania. Tanzania is stinking with corruption,"

"This would not only lead to collapse of the now-sensitive 30-year-old union between the twin-islands of Zanzibar and Pemba and Tanzania mainland, but would also plunge the country into chaos," (talking about condoning religious differences and tribalism)

Monday, June 11, 2007

SEMBENE OUSMANE AFARIKI DUNIA


Muasisi wa utengenezaji filamu barani Afrika, Sembene Ousmane amefariki dunia mwishoni mwa juma lililopita baada ya kuugua kwa muda mrefu. Alikuwa na umri wa miaka 84.


Sembene ndiye mwafrika wa kwanza kutengeneza filamu barani Afrika. Alikuwa mmojawapo wa wa waanzilishi wa tamasha la filamu Afrika, FESPACO. Alikuwa pia ni mtunzi wa vitabu. Kwa wale waliosoma somo la kiingereza wakiwa sekondari bila ya shaka walisoma pia kitabu cha God's Bits of Wood alichokiandika huyu mzee.


Binafsi nilivutiwa na kitabu hicho. Kadhalika nilivutiwa mno na filamu yake ya mwisho aliyoitengeneza, Moolaade. Mara baada ya kuiangalia nilieleza utamu wake kwenye blogu hii takriban miaka miwili hivi iliyopita.


Ameacha pengo lisilozibika - au pengine akiwa kama alama ya zama za filamu za mwanzo barani Afrika pia anafunga pazia la zama hizo - hasa kutokana na mabadiliko ya haraka yanayotokea katika utengenezaji na hadhira ya filamu za kiafrika barani hivi sasa.

Friday, June 01, 2007

MRADI WA KUIMARISHA SHUGHULI ZA BLOGU

(Maggid Akiwa katika outreach projects. picha na Maggid Mjengwa)
1
Global Voices hivi sasa wanapokea proposals za miradi ya uimarishaji shughuli za blogu. Bila ya shaka wengine wetu wameshaanza shughuli hii ya uimarishaji uandishi wa kiraia bila ya msaada wowote.

Hata hivyo haidhuru kama utapatikana msaada zaidi kidogo ili kurahisisha mambo.

Endelea hapo chini, kama unaweza kufuatilia kabla ya tarehe 15 juni fanya harahara.

Application Deadline: June 15, 2007

Rising Voices, the outreach arm of Global Voices, is now accepting project proposals for the first round of microgrant funding of up to $5,000 for new media outreach projects. Ideal applicants will present innovative and detailed proposals to teach citizen media techniques to communities that are poorly positioned to discover and take advantage of tools like blogging, video-blogging, and podcasting on their own.
As the internet becomes more accessible to more people, as computers become cheaper, and as software applications move from the desktop to the web, the so-called digital divide seems to be narrowing. In its place, however, we see a participation gap in which the vast majority of blogs, podcasts, and online video are being produced in middle-class neighborhoods in major cities around the world.
Rising Voices aims to help bring new voices from new communities and speaking new languages to the conversational web, by providing resources and funding to local groups reaching out to underrepresented communities. Examples of potential projects include:

  • Purchasing an affordable digital video camera and teaching a group of rural students how to produce an ongoing video-blog documentary about the lives of their grandparents.

  • Organizing a regular workshop on blogging and photography at a local orphanage. Portions of the budget could be used on cheap digital cameras and internet cafe costs so that participants could describe their local neighborhoods to a global audience with text and photos.

  • Working with a local NGO or social entrepreneur so that their challenges, successes, and stories are told to a global audience.

  • Translating our new media curriculum to an indigenous language, like Quechua or Wolof, that is currently not represented in the blogosphere or "podosphere." Then use the learning modules to encourage bloggers to write in those languages.


The sky is the limit, but unfortunately funding is not. Rising Voices outreach grants will range from $1,000 to $5,000. Please be as thoughtful, specific, and realistic as possible when drafting your budgets.


Feel free to ask questions in the comments section below or by sending an email to
outreach@globalvoicesonline.org

Kiungo chenye habari nzima kipo hapa.

Monday, May 07, 2007

CHEMA HAKIDUMU

Chema hakidumu kingekupendeza
Ungawa na hamu kukingojeleza
Saa ikitimu kitakuteleza


Chema wangu babu Kibwana Bashee
Alojipa tabu kwamba anilee
Illahi Wahabu mara amtwee


Hizo beti mbili nilizikariri zamani kutoka kwenye kitabu cha Abdilatif Abdala "Sauti ya Dhiki". Na kama ninavyozikumbuka zimekuwa zinanizinga mawazoni kwa masiku kadhaa sasa.

Nimeingiwa na machungu na woga. Uwezo wangu wa kufikiri au kutatua matatizo yaliyonifika umeniponyoka. Maisha yamenikumbusha uwanaadamu wangu. Kinachonisukuma ni ule moyo wa stahamali tu. Na ninaomba nijaaliwe stahamali zaidi.

Kitambo kidogo kilichopita Mwenyezi Mungu alimtwaa kipenzi Mama yangu Mkubwa, Kadala. Marehemu Kadala nilikuwa naye karibu sana wakati wa utoto wangu.

Naam, ndio maisha. Na hapa nilipo maisha mengine yanaenda kwa kasi ya mwendo wa radi. Nakimbiakimbia, ninachakurachakura kama kuku kutwa nzima. Kukicha naanza tena kama jana. Ndio maisha.

Basi naona bora kukawia kuliko kuiwacha safari. Tupo wote safarini japo tunaonana kwa nadra bloguni. Mambo yakisawazika bila ya shaka nitaongeza kasi na huku kwenye mitandao pia.

Haidhuru. Kule kwenye kurasa za Global Voices baada ya muda kama mwezi hivi kuna muhtasari wa blogu za kiswahili uliopandishwa leo. Tafadhali tupa jicho na huko pia. Bila kusahau kuperuzi kidogo kwenye ukurasa wa Reuters Tanzania.

Saturday, March 10, 2007

WOMADELAIDE 2007

(wazawa wa Adelaide - Kaurna - wakibariki tamasha)
1

Wikiendi hii tumerejea tena kwenye moja ya matamasha maarufu ya muziki wa kimadunia katika Australia - Womadelaide 2007. Mwaka huu tamasha hili ni la 15 hapa Adelaide na kwa mara ya kwanza kumekuwa na ratiba tofauti. Katika siku tatu za tamasha hili wanamuziki wote vinara wanatumbuiza mara moja tu. Haidhuru.
1
Bila kujali joto la kiangazi wapenzi wasiopungua 70 elfu wameshaanza kuburudika ndani ya viwanja vya Adelaide botanic park na wataburudika kwa siku tatu mfululizo mpaka nyasi kugeuka vumbi.
1
Pamoja na wanamuziki wa Kiafarika kama Femi Kuti (Nigeria), Salif Keita (Mali) na Mahotella Queens (Afrika ya Kusini) magwiji wengine kutoka pande zote za dunia kama akina Asha Bhosle (India); Kronos Quartet (US); Blue King Brown (Australia); Gotan Project (France / Argentina); Lior (Australia); Lunasa (Ireland); Emma Donovan Band (Australia); na Mariza (Portugal) watatumbuiza pia.
1
Kwa upande wangu mpaka hivi sasa nimeshahudhuria maonyesho ya bendi mbili za kutoka Afrika: Mahotella Queens na Femi Kuti and the Positive Force. Na bila ubishi wowote Mahotella Queens wamenisuuza moyo vilivyo.

(Bi mkubwa wa ki-Kaurna akisoma risala ya kubariki tamasha na kuwaenzi wenye nchi)
1
Kama ilivyo mila na desturi ya hapa Australia haianzi shughuli bila kutoa heshima kwa wazawa wa nchi hii wanaotambulika kama Ma-aborijino au Indigenous people ambao walikuwa 'hawatambuliki' kama binaadamu kamili kabla ya mwaka 1967.
1
Wazawa walianza kwa kutoa heshima ya ki-kaurna (inatamkwa ga-na). Mzee wa kabila (kama anavyoonekana pichani) alianza kusoma dua za kikwao akafuatiwa na vijana waliocheza ngoma ya kubariki tamasha. (juu kabisa pichani)

MAHOTELLA QUEENS (Womadelaide 2007)

(Mahotella Queens - Womadelaide 2007)
1
Mahotella Queens ndio waliofungua dimba ya tumbuizo kwenye tamasha la 15 la Womadelaide. Baada tu ya baraka za ufunguzi, bila kuchelewa kikosi cha maajuza watatu kutoka Afrika ya kusini, Mahotella Queens walivamia jukwaa namba moja na kuporomosha vibao vyao vyote maarufu - pamoja na Kazet na Umuntu Ngumuntu. ilikuwa onyesho kabambe - kwa lugha ya wanamiziki wanasema walipiga "tight set".
12
Miye naona hii ni baraka kuwashuhudia maajuza hawa wakitumbuiza, kwani walisharitaya shughuli za muziki baada ya kupotelewa na wanamuziki wenzao watatu wakiwemo Mzee Mahlatini na West Nkosi. Naona ni baraka vile hawa madada wazee - Hilda Tloubatla, Nobesuthu Shawe Mbadu na Mildred Mangxola ndio historia ya muziki wa dansi wa Afrika ya kusini. Hawa ndio hasa waliokuwamo kwenye kuipika mbaqanga jive.
1
Na kama alivyokuwa akieleza Bibie Hilda Tloubatla akiwa jukwaani - bila kujituma, kukaza nia tena baada ya kukata tamaa na misiba pengine wasingelikuwapo ndani ya tamasha mwaka huu.

Shoo yao ilikuwa swafi sana - walikuwa na mpigaji gitaa zito, mpiga gitaa, mpiga ngoma (yaani "drums") na mpiga kinanda tu. Hata hivyo vibibi hivi vilitoa vichekesho na mawaidha kwa wanawake na wanaume.
1
Usia ambao pengine haukuwafikia vizuri watoto wadogo na vichwa maji wengine ni pale walipowaambia akina mama: "Mkitaka kuwa na afya na furaha, muweze kucheza kama sisi mpaka uzeeni, siri ni kujidamka alfajiri ya saa kumi, umpe mumeo staftahi, na akirejea kutoka kazini akute maakuli, basi mumeo mwenyewe atakuwa akiwahi kurudi nyumbani kila siku, na kama ana uwezo atakununulia chochote unachotaka". Ma-feminist walinung'unika na kauli.

FEMI KUTI AND THE POSITIVE FORCE (Womadelaide 2007)

(Femi Kuti akitumbuiza Ijumaa usiku 9-3-07)

Shoo nyingine ya kutoka Afrika hapa katika Tamasha ni ile ya mwanamuziki Femi Kuti wa Nigeria. Bila ya shaka hii ilikuwa ndiyo bendi kubwa kupita zote usiku wa Ijumaa. Kulikwa kuna waimbaji, wapiga midomo ya bata ya aina zote (trumpets, alto na tenor sax, trombone, nk.) wapiga ngoma wawili, wanenguaji watatu, wapiga magitaa wawili, na mpiga gitaa zito, mpiga vinanda… pamoja na Femi mwenyewe ambaye anapuliza midomo ya bata ya aina mbili pamoja na kupiga kinanda na kuimba, kuunguruma na kufoka.
1
Onyesho lake lilikuwa ni nguvu na sauti kubwa mno. Ilikuwa kama vile amefunga vipaza sauti vya shoo za rock 'n' roll au heavy metal. Niliwaona wazee wachache wakihama mistari ya mbele huku wakiziba masikio.

Shoo ya femi ilikuwa sawa na kumsikiliza baba yake - Fela. Kulikwa na mseto wa Afro-beat na jazz ya haraka haraka. Alitoa maneno makali dhidi ya Obasanjo na viongozi wengine wa Kiafrika. Kadhalika aliwasuta waafrika waliokuwapo uwanjani, na kuwahimiza kufanya kweli. Ukiopndoa kibao cha Do Your Best na Beng Beng Beng, vibao vyote vilikuwa ni vya kisiasa.
1
Huyu bwana Femi alitoa sare na ma-Aborigine katika kupuliza sax. Ma-aborigines wanajulikana kwa mtindo wao wa kupiga digderidoo (aina ya filimbi kubwa yenye sauti nzito) huku wakitumia circular breathing. Femi alionyesha umahiri huo kwa kupuliza mlio mmoja wa sax kwa dakika kama mbili na nusu bila kukata.

Pamoja na kupenda sana kuangalia wanenguaji wa kike, mtindo wa wananguaji wa Femi wa kuwapa mgongo watazamaji huku kitambaa (au kijichupi) kikiwa kinavuka na kuonyesha msamba mara kwa mara kidogo kilinifanya nifadhaike. Vinginevyo ile dansi yao maarufu kana kwamba wanafanya mapenzi na mwanamume nadhani iliwavutia wengi pamoja na wapiga picha waliojazana upande wa wanenguaji.

Baada ya onyesho nilimkuta Msenegali mmoja anayepiga muziki hapa Adelaide, Lamin, akibishana na wazungu juu ya Femi. Wazungu wanadai waliupenda sana ule muziki kwani 'the whole stage was busy, the man's got energy, oooh!" Msenegali alikuwa anadai kuwa hakuweza kuucheza mziki ule kwa filingi.

Wednesday, February 14, 2007

KWA WAPENDANAO


Kuadhimisha siku ya wapendanao, ambayo ni leo, kwa wale mnaoweza sanaa ya kuandika mashairi ya mapenzi, , mnashauriwa kushiriki kwenye shindano la mashairi ya siku ya wapendanao la sauti za dunia. Hata kama hutaki kushiriki kuandika - suuza moyo wako hapa kwa kuperuzi sehemu ya maoni palipojaa mashairi yaliyokwishatumwa.

Monday, January 01, 2007

SALAMU ZA MWAKA MPYA (2)

Kwanza tushiriki ujumbe wa text nilioupata kwenye simu dakika chache zilizopita:
1
"May ur happiness increaselike fuel prices in TZ and your worries fall like number of votes to the opposition blocks in TZ, so that ur desires be fulfilled massively like kikwete's trips abroad. May your problems vanish like TANESCO's electricity. I wish u a happy and prosperous New year 2007."
1
Halafu tuendelee:
1
Mwezi wa 'kwanza' ndio umeshawadia katika kalenda ya kirumi. Mwezi uliobeba jina la mungu mmoja wa kirumi - Janus.
1
Janus, mungu wa hekaya za kirumi, mungu wa mabadiliko na vyanzo vipya, mungu aliyebeba funguo kama inavyoonyeshwa kwenye sanaa za kirumi.
1


Janus alikuwa na wajibu wa kufungua milango, viwambaza na vyanzo vingine vingine. Alikuwa na vichwa viwili, kimoja kinatazama mbele kimoja nyuma. Alikuwa na uwezo wa kulinda milango ya kuingilia na milango ya kutokea kwa wakati mmoja. Alikuwa na wajibu wa kuweka mizani ya matumaini ya wakati ujao kwa kuangalia matukio yaliyopita.
1
Nazungumzia mwezi wa januari nikijua kuwa ni mwaka mpya wa kirumi. Nifanyeje? Nilibahatika kuongea na babu yangu, Katego, (babu yake baba yangu) mwaka 1986 kabla hajaaga dunia. Nilimdodosa kuhusu kalenda za kikwetu.
Akanitajia miezi nane tu: Omuhangara; Omwiraguzu; Omwero gwilima; Omuhingo; Omworaguzu gw'echanda; Ekimezo; Kiswa; na Olubingo.
1
Pengine mwaka wa kikwetu ulikuwa na miezi nane tu au pengine ni kwa sababu ya uzee na ugonjwa wa usahaulifu, marehemu babu hakuweza kunitajia miezi mingine. Haidhuru, miezi ya kikwetu sijui jinsi ya kuipanga kwa utaratibu unaotakiwa au kuioanisha na misimu tunayoijua. Bora nizingumzie ninalojua.
1
Kwa kawaida wengi tunajipangia malengo binafsi ya kutimiza katika mwaka mpya. Wengine tunadhamiria kuwacha kuvuta tumbako, wengine kuwacha pombe, kupunguza vitambi, kubeba vyuma, kufanya mazoezi na kadhalika.
1
Malengo mengi huwa hayatekelezwi au yakitekelezwa basi kwa siku chache tu za mwezi wa januari. Malengi hayatekelezeki pengine kutokana na kwamba tunatumia kichwa kimoja tu cha Janus, kile kinachotazama mbele bila kutumia kichwa cha pili kinachoangalia tulikotoka.
1
Binafsi yangu lengo langu la kuwacha kuvuta tumbako nimeamua kuachana nalo vile kila mwaka nakata tamaa tarehe mbili ya Januari na kuendelea kulipuliza kama kawaida.
1
Basi hivi sasa nikiangalia nyuma na mbele najiwekea lengo linalowezekana. Lengo ambalo kila mmoja anaweza kutimiza:
1
Kutenda vitendo na kuacha kuahidi yasiyoyewezekana;
Kuwa mkweli kwa nafsi - kusema tunachoamini na kuamini tunachosema;
Kutenda haki na kudai haki;
Kutunza maadili na heshima;
Kukubali kusahihishwa tunapokosea.
Na kubwa zaidi kudumisha upendo kwani tunao uwezo wa kupenda - uwezo wa kubadili hali zetu kwa mawazo na vitendo chanya.
1
Bila kusahau kutoa shukrani kwa heri na fanaka zote zilizopita mwaka 2006, binafsi ikiwamo kumkaribisha mgeni mpya katika jamaa yangu, binti niliyebarikiwa wakati tukifungafunga mwaka - tarehe 22 desemba 2006. Jina lake nimemuita Nia.
1

Nawatakia heri ya mwaka mpya. 1

SALAMU ZA MWAKA MPYA (1)

Taa zinawaka, kelele zimepungua mjini, mvua zimenyesha, umeme umerudi, lakini hicho siyo kipimo cha ufanisi kwa shirika la umeme Tanesco, hiyo ni bahati.
1
Ujumbe huo makini nimekutana nao kwenye barua pepe za kimalumbano mtandaoni. Rafiki yangu Majaliwa katutakia heri ya mwaka mpya huku akitathmini ufanisi wa serikali ya awamu ya nne hususan kuhusiana na suala la umeme kama ilivyoandikwa kwenye magazeti hivi karibuni:
1
Kwa kweli Tanesco/umeme umekua dosari kubwa sana kwa JK's first year as president . Electricity generation technology is old and the supply and retailing of energy are now over 100 years old kwa hiyo hakuna sababu yoyote inayotulazimisha sisi wa TZ kuteseka kiasi hiki (by the way, when I say this I don't mean just in terms of lost opportunities/inconvenience from rationing but the millions of dollars-probably borrowed dollars - which are being wasted could be better spent in education, health and other essential services including road maintenance and water supplies).
1
What TZ needs is an independent regulator to forecast demand/supply and inform the market of future investment opportunities. This will mean some genuine reform to current arrangement for electricity generation and supply in Tanzania. Without genuine reform and long term plans aimed at meeting the growth in demand for electricity we will keep falling back on these short-term and expensive emergency fall-back/stopgap measures kila wakati ukame or plant breakdowns occur.
1
Na Hiyo TANESCO as it stands appears to be a wounded beast being used by different players to enhance their standing in the community as they are reliant on the 15 million plus in subsidies from the government (CCM).
1
Nauliza jamani kama hao CCM wameshindwa ku-ensure that the company runs effectively and efficiently in the 30+ years that they have had a monopoly on directing board/managerial appointments what makes them think that they can start now?
1
While there are good reasons for government ownership for key strategic assets for the benefit of the country it is not clear kwamba TANESCO is actually benefiting from this.
1
A good example of a possible way forward is our next door neighbour, Kenya, where the main power generator is well run, with prices regulated by government but the company is listed on the KSE which allows it freedom raise funds and pursue market opportunities without too much interference (see www.kengen.co.ke/index.asp). By way of example, while Kenya is suffering from the same drought as TZ and Uganda, they were able to export power to Uganda to help them in their drought related electricity shortfalls!
1
Electricity supply is old technology, inasikitisha kwamba in this day and age - the information age -that we live in sisi waTanzania,who have the right climate for progress which other countries are not blessed with, bado tunababaika na mambo ambayo on the face of it can be dealt with quite easily as they are not insurmountable.
1
Lets remember this when we next exercise our democratic rights at the polls.
1
I hope you have a "brighter" 2007 - happy new year!
1
Salaam
1
Majaliwa