Wednesday, May 26, 2010

zittokabwe.wordpress.com

Ndugu msomaji, nimekuwa na blogu hapo kabla lakini sikuweza kuifanyi kazi kama invyostahili. Nimeamua kuanzisha blogu hii mpya ili liwe jukwaa la kujadiliana jinsi ya kuimarisha demokrasia nchini kwetu Tanzania, Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Karibu kwa maoni, ushauri na hata makatazo!


- Posti ya ukaribisho katika blogu ya Mh. Zitto Kabwe


Zaidi bofya hapa.


Natafuta tafuta wabunge wengine wanaoblogu – bila bila mpaka sasa...

Tuesday, May 25, 2010

Happy Africa Day...

Saturday, May 15, 2010

MKUTANO WA UANAHABARI WA KIRAIA WA GLOBAL VOICES 2010 – Santiago, Chile

Simba, Nambiza, Bwaya


Kundi dogo la wanablogu kutoka Madagaska, Afrika Kusini, Tanzania, Naijeria, Kenya na Ivory Coast wakijadili jambo.


Mkutano wa Uanahabari wa Kiraia wa Global Voices 2010 uliofanyika mjini Santiago, Chile ulipita vizuri. Nilibahatika kukutana na wanablogu wawili wa Tanzania, Christian Bwaya na Deogratias Simba ana kwa ana kwa mara ya kwanza.


Ilikuwa ni furaha tupu kwani tuliweza kuzungumza mengi kwa lugha yetu na kwa kuelewana vizuri bila ufafanuzi au maelezo mengi kama vile tunapoongea na watu kutoka nchi na tamaduni tofauti.


Katika siku zile mbili za mkutano watu wengi kutoka kila bara walieleza na kutushirikisha katika miradi yao ya uanablogu au uanahabari wa kiraia. Wengi wa watoa mada walitoka katika nchi zenye ahueni katika upatikanaji wa intaneti, yaani hawategemei migahawa ya intaneti au kompyuta za wanapofanyia kazi ili kublogu na kuendesha miradi hiyo na hivyo miradi yao ilionekana kuwa na mafanikio zaidi. Hata hivyo kutoka Afrika kuna nchi kama Liberia na Madagaska ambazo zimeweza kufanikisha miradi hiyo ya uanahabaro ewa kiraia katika hali ngumu kama yetu au pengine hali mbaya zaidi. Maelezo ya miradi hiyo pamoja maelezo mengine ya mkutano yamewekwa hapa.


Pamoja na mambo mengine mimi binafsi nilijifunza mengi katika mkutano ule. Pengine neno ‘nilijifunza’ halitoi maana sahihi, ninaweza kusema kuwa nilithibitisha hisia zangu za muda mrefu. Kwamba ili jambo lolote au juhudi yoyote iweze kufanikiwa panatakiwa kwanza pawe na visheni, nia, ikesha mipango inayoeleweka kadhalika panatakiwa pawe na ufuatiliaji mzuri na usiokoma-koma. Mambo ya bahati bahati yanawezekana kutokea lakini sio mara nyingi bahati inaweza kuzaa mafanikio ya kudumu ambayo yanaweza kubadilisha jamii au kumpa mtu au jamii nafasi inayoheshimika.


Simba, Bwaya na washikaji wa Kibangladeshi wakiwa Sao Paulo, Brazil


Simba akisikiliza au kushangaa jambo wakati wa mkutano


Picha nyingine za mkutano kama hii ya maneno au Awab zinapatikana hapa na hapa.

MITAA

Mzee akibarizi bustanini

Mwanamke wa shoka na mbwa koko
(kuna mbwa koko wengi sana Santiago!)


Moneda Palace- Hapa ndio ofisi ya rais wa Chile, anaingilia mlango wa pembeni upande wa kushoto kwa miguu kila asubuhi, na ndio hapa alipofariki Rais Salvador Allende wakati wa mapinduzi ya kijeshi mwanzoni mwa miaka ya 70.

***************

Wapendanao kila sehemu

WAPIGA RANGI VIATU




Mtindo huu wa kupiga rangi za viatu hauniridhishi. Naona kama vile mpiga rangi hujisikia vibaya. Kama ada kila mtu hubeba gazeti na kuanza kusoma pindi mpiga rangi anapoanza kazi.

TETEMEKO

Tetemeko la ardhi lililoikumba Chile halikuwa na madhara makubwa jijini Santiago kama vile ilivyokuwa sehemu za kusini. Ni nyufa tu na majengo mengi yameshafunguliwa kwa ajili ya shughuli za kawaida.

Jengo la maonyesho (Theatre/Opera house) mtaa wa Augustina.

MICHORO

Avenue Tupical Jimenez

Bella Vista - Bohemian district? pengine...


Mji wa Santiago umejaa michoro. Sijui kwa nini miji yenye mifarakano au migongano ya kitabaka watu hupendelea kuchora majengo.








Sunday, April 25, 2010

“Many women who do not dress modestly… lead young men astray, corrupt their chastity and spread adultery in society, which (consequently) increases earthquakes.”


- Hojatoleslam Kazem Sedighi, Tehran's acting Friday prayer leader


More...



Wednesday, February 10, 2010

"I'm very happy for Africa. The continent had to wait so many years for this occasion. To have South Africa hosting the 2010 FIFA World Cup is not only very good for football, but also for the whole African continent.”

- Mexican great Hugo Sanchez

Friday, January 15, 2010

"We feel deeply and profoundly that we should be there, in Haiti, with them, trying our best to prevent death,"


- Aristide, Washington Post

Monday, January 11, 2010

The plan for the Government to establish a Diaspora department in the Ministry of Foreign Affairs is welcome news.

Many countries in the developing world have long recognised that their citizens in the diaspora are the largest non-tangible, although sometimes undocumented export.

There are existing barriers that hamper investment by Ugandans holding passports of other countries. The recent recognition of dual citizenship by Uganda is a step in the right direction.

- AllAfrica